Hii biashara ilianza mwanzoni mwa karne ya ishirini miaka ya 1920s huko Marekani kupitia kiwanda kimoja kilichokuwa kikijihusisha na utengenezaji wa virutubisho vya mwili,kiwanda hicho kilianzisha mfumo wa kuwalipa fidia wateja waliokuwa wakizinunua bidhaa zao,pia iliwalipa watu waliofanikiwa kuwaingiza watu wapya katika mtandao wa ununuaji na usambazaji wa bidhaa za kiwanda hicho.Kupitia mfumo huu kiwanda hicho kiliweza kukua kwa kasi sana kitu kilichosababisha wafanya biashara wakubwa wengine wajiunge na mfumo huu na kufungua makampuni mbalimbali yaliyoanza kufanya biashara kwa kutumia mfumo huu.Mpaka sasa hivi karibia watu laki moja wanajiunga na mfumo huu wa biashara kila wiki nchini marekani,na zaidi ya watu milioni mia tisa kumi na tano wanafanya na hii biashara duniani kote
BIASHARA HII NI NINI HASA!!!!!!!
Biashara hii kama nilivyosema hapo mwanzo ni mfumo wa biashara ambao mbali na kumlipa mwanachama (member) wa kampuni pindi anunuapo bidhaa kila mwezi,mwanachama huyo pia hulipwa aingizapo mwanachama mpya na pia hulipwa kila mwezi kutokana na manunuzi ya mwezi mzima.Hii inamaanisha kuwa mbali na mwanachama kujiingizia faida ya reja reja kupitia mauzo ya bidhaa anazonunua moja moja kutoka kiwandani pia atarudishiwa asilimia flani ya manunuzi yake (bonus) kila mwezi kulingana na jumla ya manunuzi yake kwa mwezi,pia kampuni itamlipa yeye akiwa kama ''upliner'' kwa manunuzi yatakayofanywa na wanachama aliofanikiwa kuwaingiza katika kampuni lake analofanya nalo biashara.
Wanayabiashara wengi duniani wanausapoti mfumo huu,watu kama kina Robert Kiyosaki,Michael Loise,Jim Rhon,,James Mang'amba na wengine wengi ni watu waliofanikiwa kupitia mfumo na kupitia biashara hii wanajiingizia mamilioni ya pesa kila mwezi,na wanatoa mafunzo mbali mbali kuhusiana na biashara hii.
FAIDA YA BIASHARA HII.
Kuna faida mbali mbali katika biashara hii ya mtandao lakini kwa leo nitaongelea faida chache tu za mhimu mtu anazoweza kuzipata kama ataamua kuifanya biashara hii.
1 :Utafanya biashara hii hata kama ukiwa nyumbani au mahali popote.
Biashara unaweza ifanaya ukiwa mahali popote hata kama ni nyumbani,ofisini au safarini.Unaweza ifanya kupitia simu yako au komputer yako kuwasiliana na wateja wako ,kutafuta wateja au kutangaza bidhaa zako,ndio maana wanasema biashara ya mtandao ni biashara ya karne ya ishirini na moja kwa sababu hii ni biashara inayotumia mfumo wa kisasa wa kiteknolojia,haihitaji mpaka ufungue duka au upeleke bidhaa sokoni,ofisi yako ni simu yako,computer au notebook.Pia haijalishi uwe ni mama wa nyumbani mwenye majukumu ya kulea familia au mwajiriwa wa ofisini unaweza ifanya kwa mda wowote unaokua huru kwa kutafuta wateja aukujenga team yako.
2 :Inakupatia vipato vitatu kwa wakati mmoja.
Unapofanya biashara hii unajiingizia vipato vya aina tatu kwa wakati mmoja.itakupatia kipato cha rejareja kwa bidhaa unazouza,pili itakupatia bonus za kila mwezi kulingana na jumla ya manunuzi yako na pia inakupatia bonus ya manunuzi ya team uliyotengeneza,biashara tulizozizoea zinaingiza kipato cha rejareja tu,ila hii inakupatia vyote hivi.Pia unaweza endelea jiingizia mshahara kutoka katika kazi uliyoajiriwa wakati ukiendelea jiingizia vipato hivyo vitatu kutoka katika hii biashara.
NOTE ;Kila company ina vigezo vyake katika kukulipa bonus,na kiwango cha malipo hivyo inakupasa kwanza kufanya uchunguzi na kufahamu ni kampuni gani inayokufaa.
3 :Inakuingizia kipato hata kama unaumwa au upo likizo.
Utaweza jiingizia kipato hata kama unaumwa au upo likizo kupitia team uliyotengeneza.Hapa ndio faida kubwa katika hii biashara,ajira haina warrant unapougua mwajiri awezi kukuvumilia mwaka mzima,duka lako unapougua ukilifunga hakuna kipato chochote kitakachoingia,lakini hii biashara uugue au hata kama umeamua kwena likizo bado mfereji wa hela ulioutengeneza kupitia team yako utaendelea kukuingizia pesa,je ni kazi gani au biashara gani nyingine itakayokuingizia kipato hata kama haujatumia nguvu yako tofauti na hii?,ndio maana nakwambia ukifanya biashara ya mtandao unaweza kustafu hata kama bado kijana(una nguvu).
4 :Inakusaidia kuepuka makato ya kodi.
Katika ajira na biashara za kawaida unalipa kodi kulingana na mshahara au kipato unachoingiza kwa mwezi,mshahara ukiwa mkubwa na kodi inaongezeka,biashara ikiwa kubwa pia makato ya kodi yanakuwa makubwa.Hivyo ni vigumu kwa mfanya kazi kuhifadhi sehemu ya mshahara wake kwa ajiri ya maendeleo kutokana na makato na ni vigumu pia kuanzisha biashara ya duka kama huna uhakika mzunguko wa biashara utakuawa kama utakua mzuri kwa sababu TRA watakufirisi.Lakini katika hii biashara TRA utakua unawasikia kwenye redio kwani hawatakuhusu kabisa kupitia biashara hii,hii ni kwasababu bidhaa zako zinalipiwa kodi na kampuni unalofanya nalo kazi pindi zinaingia nchini hivyo hutapaswa tena kulipa kodi.
5 :Unaweza ianza biashara hii kwa mtaji mdogo kabisa.
Kila kampuni linalojihusisha na biashara ya mtandao lina utaratibu wake
wa gharama za kuanzia katika biashara hii.Hivyo ni jukumu lako kuangalia ni kampuni gani litakufaa kuanza nalo biashara kwa mtaji ulionao,lakini kitu cha msingi katika hii biashara mtaji wa kuanzia ni mdogo sana ukilinganisha na jinsi mtu anayetaka kufungua duka au biashara nyingine.Pia unauwezo wa kuukuza mtaji wako mpaka ukawa mkubwa kwa mda mfupi kulingana na malengo uliyojiwekea.
6 :Inakupa uwezo wa kuchagua ni watu gani unaohitaji kufanya nao kazi.
Biashara ya mtandao inakupa uwezo wa kuchagua watu unaowahitaji kufanya nao biashara yako,katika biashara hii utaweza kuwa huru kuchagua watu unaoona wanafaa katika biashara yako,hii itakupa nguvu ya kibiashara kwasababu utafaya kazi na watu ambao unaona wanakufaa.
7:Unapata mafanikio kupitia kuwawezesha wengine.
Je,ushawahi kupewa shukrani kwa kumpa mtu njia ya mafanikio?,je,ushawahi kuwa kioo ambacho watu wanatumia kujitathmini katika jamii yako?,na ushawahi kuwa furaha ya watu wanaokuzunguka?.Biashara hii itakuwezesha kuwa msaada kwa watu wote wanaohangaika kwa kukosa ajira,wanaolipwa mshahara mdogo,wanaopata mateso kazini na ambao wanafanya kazi ambazo hazikua ndoto zao,wote hawa utawasaidia kwa kuwapa hii fursa ili wafanikiwe wakati huo huo wakikufanya nawe ufanikiwe,inapendeza sana eeh!!!
Zipo faida nyingi sana zinazohusiana na hii biashara ila kwa leo ningependa niishie hapo,napenda kukukaribisha wewe uliyechoka maisha ya kuranda randa kutafuta kazi,unayefanya kazi katika mazingira ya mateso na wewe uliyechoka maisha ya kukaa nyumbani bila shughuri yeyote,karibu uyabadili maisha yako kwa kuongeza thamani katika jamii yako.Kwa msaada zaidi wasiliana nami BONIVENTURE JOACHIM kwa njia zifuatazo;
Simu /watsup
: 0768-308740
E-mail : bnjige@gmail.com